chuki dhidi ya uislamu

IQNA

IQNA – Miaka mitano baada ya washiriki wanne wa familia moja ya Kiislamu kuuawa kwa kugongwa makusudi na gari katika kitendo ambacho jaji amekitaja kuwa ni cha kigaidi, wanajamii katika mji wa London, Ontario nchini Kanada, wamekusanyika kuwakumbuka wahanga hao na kusisitiza upya ahadi yao ya kupambana na chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia).
Habari ID: 3482332    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/07

IQNA – Polisi wanawatafuta washukiwa baada ya msikiti mmoja katika mji wa Moncton, ulioko kusini-mashariki mwa jimbo la New Brunswick nchini Kanada, kuharibiwa kwa maandishi ya kuta (graffiti) yenye chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu. Waumini wa msikiti huo wanasema kitendo hicho ni shambulio lililolenga moja kwa moja jamii yao ya Kiislamu.
Habari ID: 3482328    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/06

IQNA – Wakazi wa kitongoji kilichopo kusini mwa Kaunti ya St. Louis, jimboni Missouri nchini Marekani, wameamka mwishoni mwa wiki wakikuta mandhari ya kutia hofu, baada ya njia za waenda kwa miguu na baadhi ya barabara kuchafuliwa kwa maandishi ya chuki dhidi ya Waislamu.
Habari ID: 3482284    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/26

IQNA – Ingawa hujuma ya kigaidi dhidi ya Msikiti wa San Diefo ilitokea umbali wa zaidi ya maili 2,000, huzuni na taharuki yake zilihisiwa moja kwa moja kote Marekani hadi kusini-mashariki mwa jimbo la Michigan siku ya Jumatano.
Habari ID: 3482267    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/22

IQNA – Tishio la mtu mmoja la kufyatua risasi dhidi ya waumini katika msikiti mmoja mjini Brisbane, Australia, limeibua malalmiko duniani kutoa ambapo shirika mashuhuri la haki za kiraia la Waislamu nchini Marekani limetoa tamko rasmi.
Habari ID: 3482230    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/12

IQNA – Visa vya chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) na mashambulizi dhidi ya Waislamu wa Marekani na taasisi zao vimeongezeka mara kumi na moja (1,000%) katika miezi mitatu ya kwanza ya mwaka 2026, na kufikia kiwango cha juu zaidi katika kipindi cha miezi 15, kwa mujibu wa ripoti mpya ya Kamati ya Masuala ya Umma ya Waislamu (Mpac).
Habari ID: 3482147    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/17

IQNA — Hujuma kubwa ilizuiwa Jumanne jioni katika Msikiti wa Kati wa Manchester, pale wajitolea waliokuwa makini walipomkabili na kumzuia mwanamume aliyeingia msikitini wakati wa swala za Tarawehe, akiwa amebeba begi lenye shoka, nyundo na kisu.
Habari ID: 3481997    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/26

IQNA – Kumeshuhudiwa visa kadhaa vya ubaguzi wa rangi na chuki dhidi ya Waislamu nchini Brazil, hali inayoashiria kuongezeka kwa tatizo la Chuki Dhidi ya Uislamu katika taifa hilo la Amerika ya Kusini.
Habari ID: 3481942    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/16

IQNA – Kundi la waharibifu limevamia Kituo cha Kiislamu cha Imam Ridha (AS) mjini Birmingham, Uingereza, katika tukio lililoibua maswali kuhusu kuongezeka kwa chuki dhidi ya Uislamu na Iran katika nchi za Magharibi.
Habari ID: 3481816    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/18

QNA – Mwanasiasa mmoja wa Marekani ameonya kuhusu kuongezeka kwa chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) katika nchi za Magharibi wakati mwezi mtukufu wa Ramadhani unakaribia.
Habari ID: 3481802    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/14

IQNA – Kuanzia unyanyasaji wa mtandaoni hadi mashambulizi ya umati na sera za kibaguzi, mwaka 2025 uliweka bayana hali ya kutisha kwa Waislamu walio wachache nchini India.
Habari ID: 3481726    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/28

IQNA – Kugundua kuwa mtoto wako amekutana na hotuba ya chuki dhidi ya Uislamu mtandaoni ni jambo linaloweza kutisha.
Habari ID: 3481704    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/23

IQNA – Dereva mmoja Mwislamu wa Uber mjini Montreal amenusurika madhara makubwa baada ya abiria kudaiwa kumtishia kwa kisu, tukio ambalo Baraza la Kitaifa la Waislamu wa Kanada (NCCM) limekemea vikali kama kitendo cha chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3481674    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/17

IQNA – Sheria mpya inayowazuia wasichana walio chini ya miaka 14 kuvaa hijabu katika shule za Austria imeibua upinzani mkali, huku makundi ya kutetea haki za binadamu yakishutumu serikali kwa kuwadhalilisha Waislamu na kuingilia uhuru wa imani binafsi.
Habari ID: 3481656    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/13

IQNA-Jamii ya wakazi na majirani wa jiji la Norfolk, jimbo la Virginia nchini Marekani, wamejitokeza kwa wingi kusafisha na kurejesha hadhi ya Msikiti wa Masjid Ash Shura baada ya kuchafuliwa kwa maandishi ya chuki, huku polisi wakiomba msaada wa umma kumtambua mtuhumiwa.
Habari ID: 3481650    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/12

IQNA – Utafiti mpya wa kitaifa umebaini kuwa Waislamu nchini Ufaransa wanaripoti viwango vya juu zaidi vya ubaguzi wa kidini kuliko makundi mengine yote.
Habari ID: 3481619    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/06

IQNA – Baraza Kuu la Waislamu Ufaransa (CFCM) limesema waumini wameshtushwa na kuumizwa sana baada ya mtu kuvamia msikiti ulioko kusini-kati mwa Ufaransa na kurarua nakala za Qur’ani Tukufu kisha kuzitupa chini.
Habari ID: 3481605    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/02

IQNA – Ripoti mpya imeonesha kuwa matukio ya vurugu na hujuma dhidi ya misikiti nchini Uholanzi yameongezeka kwa kiwango kikubwa katika kipindi cha muongo uliopita, kwa mujibu wa utafiti wa mtandao wa misikiti K9.
Habari ID: 3481554    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/22

IQNA – Jeshi la Polisi wa Kaunti ya Richland limethibitisha kukamatwa kwa mwanamume aliyeingia msikiti mmoja wa South Carolina, Marekani, wakati wa sala huku akiwa na bunduki aina ya AR-15.
Habari ID: 3481552    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/22

IQNA – Wanafunzi Waislamu katika Chuo Kikuu cha Florida Kusini (USF) nchini Marekani wamesema wanaume watatu walivuruga mkusanyiko wao wa sala ya alfajiri na kuwatendea unyanyasaji.
Habari ID: 3481550    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/21