IQNA – Watetezi wa haki za Waislamu nchini Australia wametoa wito wa kutengwa kwa bajeti mpya na ya kutosha kwa ajili ya programu za kupambana na chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia), kufuatia hatua ya Chama cha Labour kukubali sehemu tu ya mpango uliopendekezwa na balozi maalum wa kushughulikia tatizo hilo.
Habari ID: 3482509 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/19
IQNA - Waislamu nchini Australia wanahitaji mabadiliko ya kudumu ili kukomesha ubaguzi, kulingana na mwandishi wa ripoti muhimu iliyobainisha kuwa hatua kubwa zaidi zinahitajika ili kung’oa mzizi wa chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia).
Habari ID: 3482500 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/18
IQNA – Mfanyakazi mmoja Mwislamu wa vibanda vya biashara amechomwa kisu zaidi ya mara 15 ndani ya kituo cha ununuzi (mall) huko Utah, Marekani, na mtu ambaye baadaye alikiri kwa polisi kuwa alikusudia kumuua “kwa sababu ya dini yake.”
Habari ID: 3482498 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/17
IQNA – Rais wa msikiti mmoja mjini Milwaukee, katika jimbo la Wisconsin nchini Marekani, ambaye ameachiliwa huru kutoka kizuizini na Idara ya Uhamiaji (ICE) wiki hii, amesema kuwa amekuwa akilengwa kutokana na msimamo wake thabiti wa kutetea haki za Wapalestina.
Habari ID: 3482381 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/20
IQNA – Miaka mitano baada ya washiriki wanne wa familia moja ya Kiislamu kuuawa kwa kugongwa makusudi na gari katika kitendo ambacho jaji amekitaja kuwa ni cha kigaidi, wanajamii katika mji wa London, Ontario nchini Kanada, wamekusanyika kuwakumbuka wahanga hao na kusisitiza upya ahadi yao ya kupambana na chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia).
Habari ID: 3482332 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/07
IQNA – Polisi wanawatafuta washukiwa baada ya msikiti mmoja katika mji wa Moncton, ulioko kusini-mashariki mwa jimbo la New Brunswick nchini Kanada, kuharibiwa kwa maandishi ya kuta (graffiti) yenye chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu. Waumini wa msikiti huo wanasema kitendo hicho ni shambulio lililolenga moja kwa moja jamii yao ya Kiislamu.
Habari ID: 3482328 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/06
IQNA – Wakazi wa kitongoji kilichopo kusini mwa Kaunti ya St. Louis, jimboni Missouri nchini Marekani, wameamka mwishoni mwa wiki wakikuta mandhari ya kutia hofu, baada ya njia za waenda kwa miguu na baadhi ya barabara kuchafuliwa kwa maandishi ya chuki dhidi ya Waislamu.
Habari ID: 3482284 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/26
IQNA – Ingawa hujuma ya kigaidi dhidi ya Msikiti wa San Diefo ilitokea umbali wa zaidi ya maili 2,000, huzuni na taharuki yake zilihisiwa moja kwa moja kote Marekani hadi kusini-mashariki mwa jimbo la Michigan siku ya Jumatano.
Habari ID: 3482267 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/22
IQNA – Tishio la mtu mmoja la kufyatua risasi dhidi ya waumini katika msikiti mmoja mjini Brisbane, Australia, limeibua malalmiko duniani kutoa ambapo shirika mashuhuri la haki za kiraia la Waislamu nchini Marekani limetoa tamko rasmi.
Habari ID: 3482230 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/12
IQNA – Visa vya chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) na mashambulizi dhidi ya Waislamu wa Marekani na taasisi zao vimeongezeka mara kumi na moja (1,000%) katika miezi mitatu ya kwanza ya mwaka 2026, na kufikia kiwango cha juu zaidi katika kipindi cha miezi 15, kwa mujibu wa ripoti mpya ya Kamati ya Masuala ya Umma ya Waislamu (Mpac).
Habari ID: 3482147 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/17
IQNA — Hujuma kubwa ilizuiwa Jumanne jioni katika Msikiti wa Kati wa Manchester, pale wajitolea waliokuwa makini walipomkabili na kumzuia mwanamume aliyeingia msikitini wakati wa swala za Tarawehe, akiwa amebeba begi lenye shoka, nyundo na kisu.
Habari ID: 3481997 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/26
IQNA – Kumeshuhudiwa visa kadhaa vya ubaguzi wa rangi na chuki dhidi ya Waislamu nchini Brazil, hali inayoashiria kuongezeka kwa tatizo la Chuki Dhidi ya Uislamu katika taifa hilo la Amerika ya Kusini.
Habari ID: 3481942 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/16
IQNA – Kundi la waharibifu limevamia Kituo cha Kiislamu cha Imam Ridha (AS) mjini Birmingham, Uingereza, katika tukio lililoibua maswali kuhusu kuongezeka kwa chuki dhidi ya Uislamu na Iran katika nchi za Magharibi.
Habari ID: 3481816 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/18
QNA – Mwanasiasa mmoja wa Marekani ameonya kuhusu kuongezeka kwa chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) katika nchi za Magharibi wakati mwezi mtukufu wa Ramadhani unakaribia.
Habari ID: 3481802 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/14
IQNA – Kuanzia unyanyasaji wa mtandaoni hadi mashambulizi ya umati na sera za kibaguzi, mwaka 2025 uliweka bayana hali ya kutisha kwa Waislamu walio wachache nchini India.
Habari ID: 3481726 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/28
IQNA – Kugundua kuwa mtoto wako amekutana na hotuba ya chuki dhidi ya Uislamu mtandaoni ni jambo linaloweza kutisha.
Habari ID: 3481704 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/23
IQNA – Dereva mmoja Mwislamu wa Uber mjini Montreal amenusurika madhara makubwa baada ya abiria kudaiwa kumtishia kwa kisu, tukio ambalo Baraza la Kitaifa la Waislamu wa Kanada (NCCM) limekemea vikali kama kitendo cha chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3481674 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/17
IQNA – Sheria mpya inayowazuia wasichana walio chini ya miaka 14 kuvaa hijabu katika shule za Austria imeibua upinzani mkali, huku makundi ya kutetea haki za binadamu yakishutumu serikali kwa kuwadhalilisha Waislamu na kuingilia uhuru wa imani binafsi.
Habari ID: 3481656 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/13
IQNA-Jamii ya wakazi na majirani wa jiji la Norfolk, jimbo la Virginia nchini Marekani, wamejitokeza kwa wingi kusafisha na kurejesha hadhi ya Msikiti wa Masjid Ash Shura baada ya kuchafuliwa kwa maandishi ya chuki, huku polisi wakiomba msaada wa umma kumtambua mtuhumiwa.
Habari ID: 3481650 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/12
IQNA – Utafiti mpya wa kitaifa umebaini kuwa Waislamu nchini Ufaransa wanaripoti viwango vya juu zaidi vya ubaguzi wa kidini kuliko makundi mengine yote.
Habari ID: 3481619 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/06