IQNA – Sheria mpya inayowazuia wasichana walio chini ya miaka 14 kuvaa hijabu katika shule za Austria imeibua upinzani mkali, huku makundi ya kutetea haki za binadamu yakishutumu serikali kwa kuwadhalilisha Waislamu na kuingilia uhuru wa imani binafsi.
Habari ID: 3481656 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/13
IQNA-Jamii ya wakazi na majirani wa jiji la Norfolk, jimbo la Virginia nchini Marekani, wamejitokeza kwa wingi kusafisha na kurejesha hadhi ya Msikiti wa Masjid Ash Shura baada ya kuchafuliwa kwa maandishi ya chuki, huku polisi wakiomba msaada wa umma kumtambua mtuhumiwa.
Habari ID: 3481650 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/12
IQNA – Utafiti mpya wa kitaifa umebaini kuwa Waislamu nchini Ufaransa wanaripoti viwango vya juu zaidi vya ubaguzi wa kidini kuliko makundi mengine yote.
Habari ID: 3481619 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/06
IQNA – Baraza Kuu la Waislamu Ufaransa (CFCM) limesema waumini wameshtushwa na kuumizwa sana baada ya mtu kuvamia msikiti ulioko kusini-kati mwa Ufaransa na kurarua nakala za Qur’ani Tukufu kisha kuzitupa chini.
Habari ID: 3481605 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/02
IQNA – Ripoti mpya imeonesha kuwa matukio ya vurugu na hujuma dhidi ya misikiti nchini Uholanzi yameongezeka kwa kiwango kikubwa katika kipindi cha muongo uliopita, kwa mujibu wa utafiti wa mtandao wa misikiti K9.
Habari ID: 3481554 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/22
IQNA – Jeshi la Polisi wa Kaunti ya Richland limethibitisha kukamatwa kwa mwanamume aliyeingia msikiti mmoja wa South Carolina, Marekani, wakati wa sala huku akiwa na bunduki aina ya AR-15.
Habari ID: 3481552 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/22
IQNA – Wanafunzi Waislamu katika Chuo Kikuu cha Florida Kusini (USF) nchini Marekani wamesema wanaume watatu walivuruga mkusanyiko wao wa sala ya alfajiri na kuwatendea unyanyasaji.
Habari ID: 3481550 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/21
IQNA – Baraza la Imani ya Kiislamu Ufaransa (CFCM) limepinga vikali utafiti mpya wa taasisi ya Ifop, likisema utafiti huo unachochea unyanyapaa na kuendeleza chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu (Islamophobia)
Habari ID: 3481548 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/21
IQNA-Katika kikao cha maswali ya kila wiki bungeni, Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer alitangaza kuwa chuki dhidi ya Waislamu ni jambo la kuchukiza na halina nafasi katika jamii.
Habari ID: 3481542 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/20
IQNA – Mashambulio dhidi ya misikiti nchini Uingereza yameripotiwa kuongezeka kwa kasi katika miezi ya hivi karibuni, huku ripoti mpya ikihusisha ongezeko hilo na harakati za utaifa zinazotumia alama za Kikristo na za Uingereza katika vitendo vya vitisho.
Habari ID: 3481487 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/08
IQNA – Katika kipindi cha kuelekea kuanza kwa upigaji kura wa mapema, mgombea wa umeya wa Jiji la New York, Zohran Mamdani, ametetea imani yake ya Kiislamu huku akilaani “mashambulizi ya kibaguzi na yasiyo na msingi” kutoka kwa wapinzani wake, akionya kuwa chuki hizo dhidi ya Uislamu hazimlengi yeye tu bali pia takribani Waislamu milioni moja wanaoishi jijini humo.
Habari ID: 3481417 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/26
IQNA – Mtandao wa Mazungumzo ya Kiislamu nchini Norway (Islamic Dialogue Network) umezindua tovuti ya kwanza ya kitaifa ya kupambana na chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia), iitwayo stoppmuslimhat.no.
Habari ID: 3481403 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/23
IQNA- Kufuatia ongezeko kubwa la uhalifu wa chuki dhidi ya Waislamu nchini Uingereza, serikali inatarajiwa kutangaza ufafanuzi mpya wa neno “'Chuki Dhidi ya Uislamu' (Islamophobia)”—ambapo huenda likabadilishwa na kuwa “chuki dhidi ya Waislamu.”
Habari ID: 3481402 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/23
IQNA – Mwanasiasa kutoka Venezuela, Bi Maria Corina Machado, ambaye ametunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel ya mwaka 2025, ametakiwa kuomba msamaha na kujitenga na misimamo yake ya kuunga mkono ufasisti unaoeneza chuki dhidi ya Waislamu.
Habari ID: 3481353 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/11
IQNA – Polisi nchini Uingereza wameanzisha uchunguzi kuhusu tukio linaloshukiwa kuwa shambulio la kuchoma moto kwa chuki dhidi ya Msikiti wa Peacehaven, ulioko East Sussex, usiku wa Jumamosi.
Habari ID: 3481332 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/05
IQNA- Meya wa jiji la London, Sadiq Khan, amemjibu kwa ukali Rais wa Marekani Donald Trump, akimtuhumu kuwa “mbaguzi wa rangi, jinsia, wanawake na mwenye chuki dhidi Uislamu” baada ya Trump kutumia hotuba yake katika Umoja wa Mataifa kumuita Khan “meya mbaya” na kudai kuwa jiji la London linaelekezwa kwenye “sheria ya Kiislamu (sharia)”.
Habari ID: 3481286 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/26
IQNA – Moto umeteketeza msikiti katika mji wa kusini wa Hultsfred, nchini Uswidi, usiku wa kuamkia Jumanne, na kuharibu kabisa jengo hilo.
Habari ID: 3481280 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/24
IQNA – Tume ya Haki za Binadamu ya Australia imeanzisha uchunguzi kufuatia malalamiko dhidi ya Baraza la Wahindu la Australia, likiwemo Rais wake Sai Paravastu na Mkuu wa Idara ya Habari Neelima Paravastu, wakidaiwa kujihusisha mara kwa mara na matamshi ya chuki dhidi ya Uislamu kuanzia Mei 2024 hadi Julai 2025.
Habari ID: 3481273 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/23
IQNA – Wakazi wa Plainfield, jimbo la Illinois, walikusanyika Jumapili kuadhimisha siku maalum ya kumkumbuka Wadee Alfayoumi, mtoto wa miaka sita mwenye asili ya Kipalestina na Mmarekani aliyeuawa katika tukio la chuki takriban miaka miwili iliyopita.
Habari ID: 3481266 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/22
IQNA – Mjumbe wa chama cha Democratic katika Bunge la Marekani, Bi Ilhan Omar, amesisitiza utambulisho wake wa Kiislamu, akisema anajivunia kuwa Mwislamu.
Habari ID: 3481264 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/21