iqna

IQNA

IQNA- Meya wa jiji la London, Sadiq Khan, amemjibu kwa ukali Rais wa Marekani Donald Trump, akimtuhumu kuwa “mbaguzi wa rangi, jinsia, wanawake na mwenye chuki dhidi Uislamu” baada ya Trump kutumia hotuba yake katika Umoja wa Mataifa kumuita Khan “meya mbaya” na kudai kuwa jiji la London linaelekezwa kwenye “sheria ya Kiislamu (sharia)”.
Habari ID: 3481286    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/26

IQNA – Moto umeteketeza msikiti katika mji wa kusini wa Hultsfred, nchini Uswidi, usiku wa kuamkia Jumanne, na kuharibu kabisa jengo hilo.
Habari ID: 3481280    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/24

IQNA – Tume ya Haki za Binadamu ya Australia imeanzisha uchunguzi kufuatia malalamiko dhidi ya Baraza la Wahindu la Australia, likiwemo Rais wake Sai Paravastu na Mkuu wa Idara ya Habari Neelima Paravastu, wakidaiwa kujihusisha mara kwa mara na matamshi ya chuki dhidi ya Uislamu kuanzia Mei 2024 hadi Julai 2025.
Habari ID: 3481273    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/23

IQNA – Wakazi wa Plainfield, jimbo la Illinois, walikusanyika Jumapili kuadhimisha siku maalum ya kumkumbuka Wadee Alfayoumi, mtoto wa miaka sita mwenye asili ya Kipalestina na Mmarekani aliyeuawa katika tukio la chuki takriban miaka miwili iliyopita.
Habari ID: 3481266    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/22

IQNA – Mjumbe wa chama cha Democratic katika Bunge la Marekani, Bi Ilhan Omar, amesisitiza utambulisho wake wa Kiislamu, akisema anajivunia kuwa Mwislamu.
Habari ID: 3481264    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/21

IQNA – Polisi wa McKinney, Texas, walifika wiki hii katika eneo la tukio la uhalifu lililotokea katika kituo cha elimu ya Kiislamu ambacho kikundi cha kutetea Waislamu kimekitaja kuwa ni unyanyasaji wa chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3481259    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/20

IQNA – Waislamu wawili kati ya watatu nchini Ufaransa wanasema wamekumbwa na tabia za kibaguzi, kwa mujibu wa utafiti mpya unaoangazia ubaguzi mpana katika ajira, makazi, na huduma za umma.
Habari ID: 3481246    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/17

IQNA – Misikiti kote Uskochi au Scotland nchini Uingereza imeongeza kwa kiwango kikubwa hatua za kiusalama, ikiwemo kuajiri walinzi binafsi na kuweka ulinzi wa saa 24, kufuatia njama ya kigaidi iliyozimwa na ongezeko la mashambulizi ya chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3481230    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/14

IQNA – Kitendo cha kuvunjwa kwa madirisha ya Msikiti wa Taunton, nchini Uingereza, kimezua hasira na huzuni miongoni mwa wanajamii wa eneo hilo, huku polisi wakikitaja tukio hilo kuwa ni uhalifu wa chuki unaochochewa na misingi ya kidini au ya rangi.
Habari ID: 3481226    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/13

IQNA – Mashambulizi mawili ya hivi karibuni dhidi ya msikiti mmoja huko Greater Manchester nchini Uingereza yamewaacha waumini wakihisi kutokuwa salama, kwa mujibu wa Imam wake.
Habari ID: 3481189    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/06

IQNA – Uharibifu wa msikiti mmoja huko Basildon wiki iliyopita umekemewa vikali na umeibua wasiwasi mpya kuhusu kuongezeka kwa chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) nchini Uingereza.
Habari ID: 3481175    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/02

IQNA – Hujjatul-Islam Ali Taghizadeh, mkuu wa Taasisi ya Dar-ul-Quran ya Iran, amelaani vikali kitendo cha kuchoma nakala ya Qur'ani Tukufu kilichofanywa na mgombea wa bunge la Marekani, Valentina Gomez, akikitaja kama “uhalifu wa kuchukiza” unaofichua sura halisi ya chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3481155    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/29

IQNA – Kituo cha Al-Azhar cha Kupambana na Misimamo Mikali kimekemea vikali kitendo cha hivi karibuni cha kuchoma nakala ya Qur'ani kilichofanywa na mwanasiasa mmoja wa Marekani.
Habari ID: 3481147    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/28

IQNA – Kitendo cha kuivunjia heshima na kuteketeza moto nakala ya Qur’an ambacho kimetekelezwa mgombea wa kiti katika Bunge la Kongresila Marekani kwa tiketi ya chama cha kihafidhina cha Republican huko Texas, ambaye ni mfuasi wa Rais wa Marekani Donald Trump, kimeibua hasira kubwa.
Habari ID: 3481142    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/27

IQNA – Kituo cha Kiislamu cha Al-Azhar cha Kufuatilia na Kupambana na Misimamo Mikali kimelaani kitendo cha chuki kilichotokea hivi karibuni katika msikiti wa Oxford, nchini Uingereza na kuonya kwamba matendo ya aina hiyo huchochea uhasama na ni “tishio la moja kwa moja kwa mshikamano wa kijamii.”
Habari ID: 3481120    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/22

IQNA – Mamlaka za Ufaransa zimeanzisha uchunguzi kufuatia jaribio la kuchoma moto chumba cha kusalia cha Waislamu mjini Châtillon-sur-Seine, tukio ambalo maafisa wamelilaani kuwa ni kitendo cha kigaidi cha uoga na chenye chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3481095    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/16

IQNA – Mwanamke mchanga Muislamu aliyevaa hijaab ameshambuliwa na kutishiwa maisha ndani ya basi la jiji la Ottawa, Canada eneo la Kanata, katika tukio linalochunguzwa na polisi kama uhalifu unaochochewa na chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3481079    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/13

IQNA – Viongozi wa moja ya misikiti mikubwa zaidi nchini Australia wamesema wamepokea vitisho vya kuuwawa baada ya kutangazwa mpango wa kuweka vipaza sauti vipya kwa ajili ya adhana.
Habari ID: 3481059    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/09

IQNA-Australia imeingia katika kipindi kigumu cha chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia), hali iliyoibuka kwa kasi tangu kuanza kwa vita vya kikatili vya utawala wa Israel dhidi ya Gaza.
Habari ID: 3481020    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/30

IQNA – Baraza la Mahusiano ya Kiislamu ya Marekani (CAIR) limeitaka kampuni ya uwekezaji ya Sequoia Capital kumwondoa mshirika wake Shaun Maguire, kufuatia chapisho la mitandao ya kijamii lililokosolewa vikali kwa kuendeleza chuki dhidi ya Waislamu.
Habari ID: 3480934    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/12